Kuchanganyikiwa,
Kuumizwa, Kukasirishwa
Hayo
ndio maneno yaliyokuwa yanapishana kichwani mwangu wakati nilipokuwa nachukua
Biblia yangu ili nianze kuwa na muda wa utulivu na kusali. Nilijisikia kama
sina kitu kichwani kwa wakati huo kwani moyo wangu na kichwa changu vilikuwa
havikubaliani. Nilikuwa nafikiria jinsi nitakavyobishana na mume wangu juu ya
swala Fulani.
Kwanini
haoni ninamaanisha nini? Kwanini hanielewi? Kwanini anakuwa msumbufu kiasi
hicho?
Nilifunga
Biblia yangu na kuamua kuwa jambo la msingi kwa wakati huo ni kupiga magoti na
kusali. Hivyo ndivyo wanawake wanaomtumainia Mungu wanavyofanya nilijiambia
kichwani mwangu. Na kimoyomoyo nilianza kufikiria orodha ya nini ambacho ningependa
Mungu anifanyie kumbadilisha mume wangu kila kitu nilichoona kuwa si sahihi kwa
mume wangu kuwa au kufanya. Ghafla nikiwa katikati ya maombi nikaanza kuhisi
sauti ya Mungu ikiniambia “Acha”
Acha???
Niache kusali???? Hapo moja kwa moja nikagundua kuwa siyo sauti ya Mungu hivyo
nikaendelea kusali. Lakini neno “acha” likaendelea kugonga kichwani kwangu kama mapigo ya moyo wangu yalivyokuwa yanapiga. Kitambo
nikaanza kuona lazima kuna kitu si bure na nikagundua ni kwa nini. Mungu hakutaka niwe mke wa “kumbadilisha” mume
wangu. Mungu alitaka niwe mke wa “kumpenda” mume wangu.
Nilitaka
kuacha kusali, hatimaye nikabadilisha namna ya kusali kwangu. Ni kweli kuna
mambo mume wangu alitakiwa kuyafanyia kazi lakini hakuna kizuri kilichotokea
kwani muda wote mimi nilikuwa namlaumu kwa madhaifu yake.
Nilihitajika
kuwa mwanamke mwenye busara na uthubutu wa kumuomba Mungu aniongoze na
kunifundisha jinsi ya kumpenda mume wangu japo ana madhaifu yake. Nilitakiwa
nimuulize Mungu ni wapi nakosea, wapi nakuwa mbinafsi ili niweze kufanyia kazi na
kujirekebisha.
Nilipobadilisha
mwelekeo wangu na kumruhusu Mungu anibadilishe mimi ndipo nilipoona mabadiliko
kiasi.
Katika
kipindi hiki cha mahangaiko haya Mungu alinifundisha mambo makubwa matatu:-
1. Je haya ni masumbufu
au matatizo?
Kuna
tofauti kubwa kati ya masumbufu na matatizo. Nilipojua tofauti ya vitu hivyo
viwili ilikuwa rahisi kwa mimi kushinda hii vita. Kama
haya yalikuwa ni masumbufu inabidi nijitahidi kukubali kubadilika na
kukubaliana nayo, mtulivu au kuvumilia.
2. Je ninaomba kwa
ajili ya mume au ninamuombea mume?
Ninapoona
kuna kitu kinatakiwa kubadilika kwa mume wangu basi hapo ninatakiwa kumuombea
na si kuomba kwa ajili yake. Kuomba kwa ajili yake ni kuonyesha kuwa hupendezwi
naye hivyo unataka abadilike. Wakati kumuombea ni kumuomba Mungu atengeneze
pale anapoona panahitaji marekebisho. Tunapoomba kwa jina la Mungu tunaomba
MAPENZI yake Mungu yatimizwe na kamwe si mapenzi yetu.
3. Mwelekeo wangu uko
wapi?
Siwezi
kuwa na mamlaka ya kudhibiti mtu fulani kufanya jambo fulani, lakini nina uwezo
wa kujidhibiti nisifanye jambo fulani. Mwelekeo wangu hautakiwi kutafuta mwenza/mume
aliye mkamilifu bali mwelekeo wangu unatakiwa kuwa mimi niwe mwenza/mke
mkamilifu.
Taratibu
kadri nilivyoendelea kuondoa moyo wangu kwenye maeneo hayo nimeanza kuona
mabadiliko kwenye ndoa yetu. Je bado napata
makwazo, nachanganyikiwa, naumia? Bila shaka ndio. Lakini pale nilipoacha
kujaribu kumtengeneza au kumbadilisha; nilibadilishwa mimi na kuanza kumpenda
jinsi alivyo tena kumpenda kikamilifu kama
maandiko yanavyotufundisha katika Waefeso 4:2
Muwe daima wanyenyekevu, wapole na
wenye saburi; vumilianeni ninyi kwa ninyi kwa mapendo
Nimegundua
kuwa kumpenda mume wangu ni raha na rahisi sana zaidi ya kujaribu kumtengeneza!!!!
Mwenyezi
Mungu, nisaidie kuwa na mwelekeo wa kuwa mke mwema, usiufanye moyo wangu kuwa
mgumu. Nisaidie kuziacha fikra zangu na kukusikiliza wewe pale unaponena nami
mambo mema yatakayoimarisha ndoa yangu. Katika jina la Yesu ninaomba na
kushukuru Amen
Shukrani
kwa rafiki zangu wapenzi Irene Mlola, Lilian Madeje na Evelyn Madeje….. You are
the best friends I have in my life. Stay blessed.
No comments:
Post a Comment