Wednesday, 9 November 2011

Mambo 50 yanayoweza kukufurahisha

Jumamosi iliyopita nilikuwa nje ya Dar es salaam kwa mapumziko, kule nilikuwa na mume wangu mpenzi ukweli nikaanza kujiuliza "hivi tofauti na kutoka na mume wangu ni nini kingine napenda ambacho huwa kinanipa furaha na hii ndio list yangu



1. Kupata hela kama noti ya 10,000/= kwenye nguo ya zamani (wakati umechalala)

2. Kuwa na sikukuu katikati ya week (siku za kazi)

3. Kulala kwenye mashuka fresh kitandani kwako (hasa wanaume wanapenda hii)

4. Kuogelea (Kama siyo muoga kama mimi)

5. Kusikia neno nakupenda kutoka kwa umpendaye

6. Kupumzika kwenye kijua cha asubuhi (ambacho siyo kikali sana)

7. Kupokea maua au chocolates mara kwa mara kutoka kwa mtu fulani (unayempenda ofcourse)

8. Kupata ujumbe (sms) za mahaba kutoka kwa umpendaye

9. Kukumbatiwa (pale unapojisikia)

10. Kutumiwa ujumbe/ kadi ya shukrani kutoka kwa mtu uliyemsaidia

11. Kuwaona wazee (Bi/ Bw.) wameshikana mikono (unatamani ingekuwa wewe na umpendaye)

12. Kuendesha gari huku unasikiliza muziki kwa sauti ya juu kidogo

13. Kushinda bahati nasibu hata kama ni ya Tsh. 20,000/= (kama unashiriki)

14. Kupanga mambo ya likizo (hasa ya mwisho wa mwaka)

15. Kusikiliza muziki unaoupenda sana (mimi ningesikiliza You are still the one wa Shania Twain)

16. Kupata kitu kwa bei ya punguzo

17. Kukutana ra rafiki wa zamani hasa utotoni (Ooh hii naipenda sana... come on old friends where are you)

L-R : Lulu, Irene,Flora, Rehema & Juliana

18. Kwenda kutembea mbugani, ufukweni nk

19. Kupandishwa cheo kazini (Haaa haaa hasa mshahara ukipanda lol)

20. Kwenda matembezi ya jioni na umpendaye (Dinner for two i real like it)

21. Kusikiliza muziki ambao utakukumbusha mambo yako ya zamani (Mi huwa nikisikiliza Mwanameka na Mayasa duh sisemi)

22. Kuangalia picha za zamani (Nina picha yangu nikiwa some months old naipenda sana)

                                                               Baby me haaaa haaaaa

 23 Kupata marafiki wapya (Kwa facebook nimepata marafiki kdhaa wa ukweli Da Fiona!!!!)

24. Kuwa na muda wako binafsi (ukitaka kulala hayaa.. ukitaka kucheza hayaa bora ni wewe peke yako)

25. Kuwa mzazi mtarajiwa (Mimi kuwa na mimba napenda sana)

26. Kusikia ki/vicheko vya watoto (hasa wakiwa watoto wako)

27. Kuwa na usiku wa wadada/ wakaka kutoka peke yao (japo ruhusa huwa ngumu)

28. Kuamka asubuhi na kugundua kuwa ni Jumamosi (Yuhuuuuuu its Saturday)

29. Kunywa kitu unachokipenda sanaaa ( Kwangu mimi ni Fanta ya baridi)

30. Kula kitu unachokipenda sana (Kwangu mimi ni samaki)

31. Kuweza kuvaa jeans ambayo hapo awali haikuwa ikikutosha (Hasa kama umepungua unene lol)

32. Kusifiwa na mkuu wako wa kazi (Boss)

33. Kusikia harufu nzuri ya mikate na keki inayookwa (Pita shoprite kule bakery utajua)

34. Kufanya pedicure (Hasa kupata ile massage aahaaa i like it)

35. Mtu kukwambia kuwa umepungua uzito (Heee heee niulizeni ninavyopata bichwa nikiambiwa hivyo)

36. Kugundua kuwa kuna mtu anapenda sana kufanana na wewe kila kitu (Nani anapenda kuwa kama mimi?)

37. Kwenda sinema ukiwa na umpendaye au company ya nguvu

38. Kurudi kwa umeme hasa kama ulikuwa hutarajii urudi saa hizo (utasikia huoooooo)

39. Kufika mwisho wa safari kama unaenda mapumziko (Zanzibar, Bagamoyo, Mwanza.......)

                                                      Malaika Beach Resort - Mwanza
40. Kutengeneza nywele hadi ujihisi umependeza (Inakujengea ujasiri wa hali ya juu)

41. Kukuta bank account yako ina hela (hata kama hujui nani kakuwekea)

42. Kupata leseni ya udereva/ Passport

43. Kukaa kwenye hoteli ya kifahari

44. Kuambiwa na wanao kuwa wanafanya vizuri darasana (na hasa ikija report ya shule)

45. Upo kwenye daladala umesimama umechoka halafu abiria uliyesimama pembeni yake awe anashuka kwa hiyo wewe unapata nafasi

46. Mtu kukurushia muda wa maongezi (Tigo rusha, Voda fast. Airtel................. )

47. Kulala huku kuna kamvua kananyesha na ka-ubaridi kwa mbali

48. Kupata kinywaji cha baridi baada ya kumaliza kazi (Juice, Soda, beer and Wine)


49. Kuwa muumini mzuri wa dini yako

                              My Bible School Certificate na bado naendelea...... God bless me!!!

50. Kubwa kuliko yote ni KUPENDWA (Jamani ukijua unapendwa ni RAHA acheni tu)

Wewe unafikiri nini juu ya hii list? kuna chochote kilichopungua unadhani kingekuwepo? Kama kipo tafadhali kiweke kwenye maoni yako hapo chini.


No comments:

Post a Comment