Thursday, 29 March 2012

Maombi kwa ajili ya Ndoa yangu



Mungu nisaidie ili niwe mke mwema kwa mume wangu, Ninajua fika siwezi kuwa mke mwema bila wewe kuhusika kunifanya kuwa hivyo.

 Ondosha ubinafsi wangu, makwazo yangu, na kukata kwangu tama na ubadilishe kuwa uvumilivu na utayari wa kuyakubali yote.

Ondosha tabia zangu za hasira, hisia, kujihami na unifanye mwenye uvumilivu, huruma, mwema, mwaminifu, mpole na mwenye kujiamini

Ondosha ugumu wa moyo wangu na uvunje kuta za kuteseka kwangu. Uniumbie moyo safi na uniwekee mapenzi, amani na furaha ndani yake.

Najua peke yangu siwezi baba ila ni kwa msaada wako tu.

Nionyeshe dhambi zangu zinapojidhihirisha moyoni mwangu na hasa pale inapomuhusu mume wangu mpenzi. Ninakiri kuna wakati sikuwa na mapenzi naye, nikiwa na chuki naye, hasira naye na hata kumdharau na kutomjali kama mume wangu na kutomsamehe kwa pale aliponikosea.

Baba naomba uniponye maumivu ya moyo wangu pale nilipoumizwa na mume wangu, uzipoze hasira zangu na unipe ujasiri pale nilipokata tama na unisaidie kumsamehe hata kama hajaniomba msamaha kama wewe unavyonisamehe na kamwe huwa hukumbuki maovu yangu.

 Baba nakuomba unifanye mimi kuwa chombo cha suluhu, amani na uponyaji wa ndoa yangu na mume wangu.

Baba naomba utusaidie mimi na mume wangu tuweze kuwasiliana vizuri na kuepukana na pepo wa kutengana anapojisogeza kati yetu. Mfanye mume wangu kuwa mwenzangu, rafiki yangu, kiongozi wangu, baba wa watoto wangu na msaada wangu na kwa familia yetu kwa ujumla.

 Nisaidie niweze kutengeneza mazingira mazuri ya amani, furaha, salama na upendo ili hata yeye atamani kurudi nyumbani na kukutana na hayo mambo mazuri.

Baba nakuomba unifundishe jinsi ya kujitunza ili niweze kuendelea kuwa na mvuto kwake kama mke. 

Ee baba unikuze niwe mwanamke mbunifu na mwenye kujiamini ambaye nitakuwa tajiri wa fikra, akili, roho na moyo. Nifanye niwe mwanamke ambaye mume wangu atajisikia ufahari kusema mimi ni “mke wake” mbele ya wenzake.

 
Baba nayaweka matarajio na maombi yangu yote msalabani ili ukashughulike nayo.

Ninamuachia mume wangu kutoka kwenye mzigo wa kwa kunitimizia yale niliyofikiria ni yeye pekee anaweza kuyatimiza nakuletea wewe baba ili unitimizie

Unisaidie kumkubali jinsi alivyo na wala si kumbadilisha, nimegundua kuwa kwa kiasi fulani hawezi kubadilia lakini pia kwa wakati huo huo nakukabidhi umbadilishe kwa kadri ya upendavyo wewe kwa kiasi ambacho sijawahi kufikiria anaweza kubadilika.

Ninaacha mikononi mwako mabadiliko yoyote utakayoona wewe yampasa kubadilika, ninamkubali vyovyote alivyo kwani hakuna aliye mkamilifu kati yetu bali wewe BWANA usiyebadilika ndiye mkamilifu na nina imani utatufanya sisi kuwa wakamilifu kadri ya mapenzi yako.

Baba ninaomba unifundishe jinsi ya kuomba kwa ajili ya mume wangu na ufanye maombi yangu kuwa lugha sahihi ya mapenzi yetu.

Pale mapenzi yalipokosa nguvu baba tengeneza upya mapenzi kati yetu. Nionyeshe mapenzi ya kweli yalivyo na jinsi ya kuwasiliana naye ili naye aweze kunielewa.

Jenga umoja na mshikamano kati yetu ili tuweze kukubaliana kwa kila jambo. Mungu wa uvumilivu, Mungu wa ustahamilivu na Mungu wa Faraja utajalie mawazo yetu yawe sahihi kwa kila mmoja kwa jina jina la Yesu.

Utufanye sisi kuwa wamoja wala usitutenge, usitufanye washindani, usitufanye kila mtu ashike lake bali utufanye kuwa wamoja, tusihesabiane madhaifu ya kila mmoja wetu wala makosa yake ili tuwe na mahusiano yenye upendo na amani.

Utusaidie baba tujadili kwa amani yale yenye maana na kutujenga tu; kwa yale yenye kuumiza na kuturudisha nyuma baba tunaomba uyaondoshe kwetu.


Baba ninaomba viapo vyetu kwa kila mmoja wetu vizidi kustawi na mapenzi yazidi kuongezeka siku hadi siku..

Msaidie mume wangu awe ndio kiongozi na kichwa cha familia yetu kama ulivyomfanya kuwa toka kwenye ile bustani ya Eden. Baba uniwezeshe niweze kumsaidia, kumuwezesha na kumuheshimu.  Niwezeshe kuelewa ndoto zake na matamanio yake kadri anavyotamani kuwa. Nionyeshe matakwa yake na mahitaji yake na pia unionyeshe kabla hayajajitokeza ili niwe na suluhisho. Baba  rudishsha uhai kwenye ndoa hii wala isiteteleke tena.

Baba unifanye mtu mpya, baba unipe mtazamo mpya, na mtazamo chanya na uhusiano ulio imara na mwanaume uliyenipa. Nisaidie nimuone kwa jicho jipya, mapenzi mapya na kumkubali upya.

Mpe mume wangu MKE MPYA na mke huyo awe ni mimi Lulu na si wala mwingine.

Ninaomba haya katika Kristo Bwana na Mwokozi wetu AMEN



…………….....................................................………………………………

10 comments:

  1. Nimeipenda hii sala. Naomba kupokea mafundisho mengine yahusuyo ndoa kama yapo. Ahsante!

    ReplyDelete
  2. Mungu tusaidiane sisi wanawake tulio ndoan upokee sala za unyonge wetu

    ReplyDelete
  3. i love it... nimeisoma na hisia zote kama mm ndio ninayoiomba asante mtoa maombi haya

    ReplyDelete
  4. Amen, sala nzuri sana ina leta hisia na uhalisia wa kweli, be blessed

    ReplyDelete
  5. Amen na naamini imekuwa kama nilivyoomba asante Yesu

    ReplyDelete